Home » , » DONDOO FUPI ZA KIKAO CHA MYIC 14/06/2015

DONDOO FUPI ZA KIKAO CHA MYIC 14/06/2015

Written By binally on Sunday, June 14, 2015 | 4:13 PM



MUHTASARI MFUPI WA KIKAO CHA JUMUIYA
14/06/2015
MUBAARAK CONFERENCE HALL

v  Kikao kilifunguliwa kwa dua saa 10:52 jioni na wajumbe kukaribishwa kikaoni kisha kutajwa ajenda za kikao.

AJENDA ZA KIKAO
*  Mchakato wa vitambulisho
*  Usajili wa jumuiya
*  Akaunti ya jumuiya
*  Uundaji wa kamati kuu
*  Mapato na matumizi
*  Mahudhurio vikaoni
*  Ushiriki katika matukio ya wanajumuiya
*  Miiko na maadili
*  Mustakbali wa jumuiya
*  Mengineyo:
·         Bodi ya wadhamini
·         Vyanzo vya mapato n.k

v  Mchakato wa Vitambulisho
Vitambulisho tayari vilishakuwa katika mchakato wa kuvitoa na kilichopelekea kukwama ni
a.       technical problem katika upande wa CAMERA, ambapo ziligoma kuonesha picha kwa upande vitambulisho vya viongozi kwa camera zote mbili zilizotumika hivyo kukawa na uzito.
b.      Kupiga passport wakiwa na sare ya aina moja kwa akina dada ambapo zoezi hili lilishindikana kufanyika ktk kikao cha tarehe 26/10/2014
Hata hivyo zoezi bado lipo katika mchakato na kikao cha jumapili 21/06/2015 litafanyika zoezi la upigaji picha.

v  Usajili wa jumuiya
Katika usajili tulishindwa kutimiza baadhi viambatanisho muhimu ambavyo ni sehemu ya masharti ya usajili na kutojua umuhimu wa kusajili jumuiya na faida zake,hivyo kupelekea kusuasua kwa zoezi hilo. Hata hivyo kutokana na hali ilivyo hivi sasa ya kuwa lazima tutambulike kwanza na taasisi fulan ndio tupate usajili, uongozi sasa unalazimika kutafuta njia rahis na isokuwa na vikwazo ili kusajili jumuiya hii ili kuepukana na urasimu uliopo.

v  Ufunguzi wa akaunti
Mchakato tayari ulishafanyika na kila kitu kilishakuwa tayari toka mwezi 11 mwaka jana juu ya ufunguzi wa akaunti ambayo itakuwa na jina la jumuiya yaan MYIC Account. Zoezi hili lilikwama baada ya kupata mkanganyiko wa taarifa;
a.       Mwanzo tuliambiwa kufungua akaunti kuna hitaji majina ya viongoz wa 3, picha zao pamoja na muhutasari wa kikao kinnacho ambatana na saini za wanajumuiya wote, ila tulipo kamilisha hili tukaambiwa akaunti itakayofunguliwa ni joint venture account amabyo haitakuwa na jina la jumuiya hivyo tukafeli.
b.      Sasa ili kufungua account yenye jina la jumuiya ni lazima jumuiya isajiliwe nan do utaratibu ambao umewekwa na wizara ya inayosimamia mashirika binafsi inavyosemekana, kwa hiyo hili nalo tukafeli kwakuwa hatuna usajili.
Kinachofanyika sasa ni ufuatiliaji ktk benki ya NMB tumedokezwa tunaweza kusajili bila ya usajili hivyo tupo katika kufuatilia.


v  UUNDAJI WA KAMATI KUU
Kutokana na umuhimu wa kamati hii ilikuwa iwe tayari toka siku nyingi na ilikuwa ni moja ya ajenda ktk kikao cha trh 26/10/2014 ila haikujadiliwa kiundani zaidi ya kuongeza idadi ya wajumbe kutoka wa 3 mpaka wa5 ili kuleta uwiano sawa na idadi ya viongoz ndan ya kamati hiyo ili yapatikane maamuz yasiyo na upendeleo. Hivyo kikao cha leo kimefanikiwa kuwapata hao wajumbe watano waliopitishwa na wanajumuiya wenyewe kwa hiari zao. Wajumbe hao ni;
1.      FAIDHA MWANYEMBA
2.      KULTHUM HASSAN
3.      MWANAKHATIBU OMAR
4.      HUSSEIN SENDARO
5.      HASSAN WAZIRI

v  MENGINEYO
Kutokana na muda ililazimika kujadili ajenda ya mengineyo ambapo mengi yalisemwa ;
A.    Kwann sherehe ya Ibrahim Masoud ilisimamiwa na wana mubaark na si jumuiya?
JB: tangu kupatikana kwa katibu, jumuiya haijihusishi na kuigharamia sherehe kwa ujumla wake ila ni utoaji wa zawadi na cheti cha pongezi na vilifanyika, na jumuiya pia ilikaa kikao trh 29/04/2015 kujadili uendeshaji wa hiyo sherehe hivyo jumuiya ilishiriki.
B.     Nini kimetokea kufanya jumuiya ifike hapa ilipofika?
JB: yapo mengi yalotokea ila sasa ni wakati muafaka kwa viongozi kujibu hoja kivitendo na kuacha blablah!

v  MAJUMUISHO NA KUFUNGA KIKAO
a.       Kila mwanajumuiya atatumiwa taarifa za madeni yake na atatakiwa kuonesha ushirikiano katika hili
b.      Kamati kuu itakutana ndani ya wiki hii ili kufanya maamuzi magumu kwa maslahi ya jumuiya na wanachama
c.       Itatumika orodha ya waliofika leo kuwapa taarifa kwa ajili ya kukutana jumapili ijayo kwa kuendelea na jenda zilizobaki.
d.      mahudhurio ya kikao kijacho ndo yatatumika  kama chujio la kuwachuja wasio kuwa active. Kutokuhudhuria ndio kujivua uanachama.
e.       Kikao kimeahirishwa mpaka jpili saa 3:00 asubuhi
Share this article :

+ comments + 1 comments

June 16, 2015 at 5:41 AM

Special thanks to our Secretary General for his clarification

May Allah give him strength to overcome all leadership challenges

Regards.

Post a Comment

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. Mubaarak Youth Islamic Community - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger