Home » » JE wajua WE MWANAMKE

JE wajua WE MWANAMKE

Written By binally on Sunday, April 20, 2014 | 9:47 PM


Kuwa Mwenyezi Mungu Subhanahu wa Taala amekuamrisha kuvaa Hijabu?
Mwenyezi Mungu anasema;
“Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu (SAW)! Waambie wake zako, na binti zako, na wanawake wa Kiisalamu wajiteremshie uzuri nguo zao. Kufanya hivyo kutapelekea upesi wajulikane (kuwa ni watu wa hishima ili) wasiudhiwe. Na Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe (na) Mwingi wa kurehemu.”
Al Ahzab = 59

Je! Mnazijuwa sifa za hijabu walokuwa wakivaa Masahaba wanawake (RA)?
Anasema Aisha (RA);
“Mtume wa Mwenyezi Mungu (SAW) alikuwa akeshamaliza kusalisha sala ya asubuhi (Alfajiri) wanawake huondoka wakiwa wamejifunika vitambaa vyao hawajulikani kutokana na giza wala hawatambuani wenyewe kwa wenyewe.”
Bukhari na Muslim

Je unajuwa kuwa kuonyesha mapambo ni katika matendo ya wakati wa ujahilia?
Mwenyezi Mungu anasema;
“Na kaeni majumbani mwenu, wala msionyeshe mapambo yenu kama walivyokuwa wakionyesha mapambo yao wanawake wa zama za ujahili (zama za ujinga – ukafiri).”
Al Ahzab – 33

Je unajuwa kuwa kujifananisha na makafiri kwa mavazi kunakufanya uwe mfano wao?
Mtume wa Mwenyezi Mungu (SAW) amesema;
“Atakayejifananisha na kaumu yuko pamoja nao.”
Ahmed na Abu Daud – na hadithi hii ni njema.

Je unajuwa kuwa Pepo imeharamishwa kwa wenye kuonyesha mapambo yao?
Mtume wa Mwenyezi Mungu (SAW) amesema;
“Aina mbili ni watu wa motoni sijapata kuwaona: Wanawake waliovaa huku wakenda uchi, wanayumba wakiyumbisha, vichwa vyao mfano wa nundu la ngamia lililoelemea upande mmoja. Hawatoingia Peponi wala hawataionja harufu yake.”
Muslim

Je unajuwa kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (SAW) amewalani wanawake wanaojifananisha na wanaume?
“Mtume wa Mwenyezi Mungu (SAW) amewalani wanaume wanaovaa nguo za kike na wanawake wanaovaa nguo za kiume.”
Abu Daud na Ibni Majah na hadithi hii ni sahihi.

Je unajuwa kuwa haijuzu kuvaa nguo nyepesi?
Mtume wa Mwenyezi Mungu (SAW) alisema kumwambia Osama bin Zeid;
“Mbona hujakivaa kile kitambaa kilichotoka Misri?”
Akasema;
“Nimempa mke wangu.”
Mtume (SAW) akamwambia;
“Mwambie  avae shumizi chini yake  kwani naogopa isije ikabainisha umbile lake.”
Ahmed na Al Baihaqiy na hii ni hadithi njema

Je unajuwa kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (SAW) ameamrisha kuacha kujipamba na kujipaka mafuta mazuri wakati wa kutoka?
Mtume wa Mwenyezi Mungu (SAW) amesema;
“Msiwazuwie wanawake kwenda misikitini, (lakini) watoke bila kujipaka mafuta mazuri.”
Muslim

Je mnajuwa kuwa kujipaka mafuta mazuri mbele ya wanaume ni sawa na kuzini?
Mtume wa Mwenyezi Mungu (SAW) amesema;
“Mwanamke yeyote atakayejipaka mafuta mazuri kisha akapita mbele ya kundi wakaisikia harufu yake anakuwa keshafanya kitendo cha zina.”
Abu Daud – Attirmidhiy – Annasai na hadithi hii ni sahihi

Je unajuwa kuwa mwanamke wa kiislamu hapigani vikumbo na wanaume?
Mtume wa Mwenyezi Mungu (SAW) alitoka msikiti akaona mchanganyiko wa wanawaume na wanawake njiani.
Mtume (SAW) akasema;
“Jichelewesheni kwani haipasi kwenu kupita kati kati ya njia, piteni kando ya njia.”
Wanawake wakawa wanakwenda wakijibana na ukuta hata nguo zao zilikuwa zikiganda ukutani kutokana na kujibana kwao.
Abu Daud – hadithi njema
Share this article :

Post a Comment

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. Mubaarak Youth Islamic Community - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger