Home » , » FALSAFA YA MAISHA YA MUISLAMU I

FALSAFA YA MAISHA YA MUISLAMU I

Written By binally on Tuesday, April 15, 2014 | 2:26 PM




MAISHA YA MUISLAM
Mwanadamu katika maisha yake yote hana budi kufahamu ana jukumu gani akiwa kama mwislamu katika dunia hii. Suala hili linakuja pale mwislamu anapojitambua (self-actualization) na kujitambua hakuwezekani mpaka mwislamu huyu ameweza kujibu maswali haya:-
*      Mimi ni nani?
*      Ninatoka wapi?
*      Niko wapi na kwanini?
*      Ninaelekea wapi?
*      Mwisho wangu utakuwa nini?

Haya ni ndio tunayoyaita maswali ya msingi. Mwislamu anapoweza kujibu maswali haya na akazingatia majibu yake tunasema mtu huyo amejitambua iliyobaki ni kutekeleza tu katika utendaji wa kitu chochote kujitambua ndio jambo la msingi la kwanza kabisa. Kwa mfano: Meneja hawezi kuwa meneja mzuri kama hajitambui kwa maana kwamba haelewi ilikuwa meneja mzuri anatakiwa awe vipi na afanye mambo gani yanayomwajibikia, vivvyo hivyo muislamu hawezi kuwa muislamu safi kama haelewi aweje na aishi vipi.
Katika Makala hii tutajaribu kutoa maelekezo ya majibu fasah ya maswali haya ya msingi yanayomuwezesha muislam ajitambue na aishi kweli kama muislamu.

MIMI NI NANI?

 

Mtu anapoulizwa wewe ni nani mara nyingi hukimbilia kutaja jina lake. Kwa mfano: akasem mi ni kibabu, juma,zawadi,zainabu au kandoro. Lakini ukweli ni kuwa yeye si kibabu, si juma, si zawadi au kandoro kwani hili ni jina tu, kama ilivyo kwamba anashati,suruali, gauni na viatu.Sasa gauni, shati, suruali na viatu ambavyo vyote ni vyake tukiviweka pembeni yeye anabaki kuwa ni NANI? Kwa sababu kama ambavyo anaweza kubadilisha shati lake ,gauni au suruali na vitu vingine na jina pia anaweza kubadilisha. Yeye ni kile kisichoweza kubadilika. Vilevile anaweza kujibu mimi ni MTU. Bado jibu hili sio sahihi sana kwa vile hata UTU anaweza asiwe nao pia akawa na tabia za kinyamatu.Hivyo utu pia hubadilika hivyo mtu atatoa jibu fasaha na sahihi lisilo na utata kama atajibu mimi ni KIUMBE. Mtu anapojitabulisha kwamba ni kiumbe ni wazi kuwa anatambua asili ya kiumbe chochote kile ni kuumbwa na kukubali kwake kuwa kiumbe ni wazi kuwa anakubali yeye kaumbwa. Na ili ajitambue vyema ni lazima afahamu kaumbwa na nani. Hii ni wazi kwani hata mtoto mdogo hutambua kuwa amezaliwa na anapojitambulisha vizuri humtaja baba yake. Kiumbe anayejitambulisha vyema humjua muumba wake, SISI waislamu tunatambua muumba wetu ni MWENYEZI MUNGU (SW) hata watu wengine ambao sio waislamu wanatambua kuwa yupo muumba ingawa wanapuuzia ukweli huu au kumshirikisha.

NINATOKA WAPI?
itaendelea..........

Share this article :

Post a Comment

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. Mubaarak Youth Islamic Community - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger